9.5 C
London
Friday, October 18, 2024
HomeInternationalKENYAMwezi Mtukufu wa Ramadhani

Mwezi Mtukufu wa Ramadhani

Date:

Related stories

African Peacebuilding Network: Individual Research Fellowships

The APN and Next Gen program of the Social...

Applications for IOC Young Leaders Programme 2025-2028 now open

Applications for IOC Young Leaders Programme 2025-2028 now open Young...

Turmoil in Kenyan Politics; National Assembly Votes to Impeach Deputy President.

In a stunning development that has sent shockwaves through...

How Can African Women Bridge the Digital Gender Gap?

By Guest Writer There is a harsh reality in digital development:...

Man, 47, jailed for FGM in Nottingham

The UK is making strides in sending perpetrators of...
spot_imgspot_img
Reading Time: 3 minutes

Ramadhani ni mwezi mtukufu ambao waislamu hutumia mwezi huu kama wa ibada wakiwa wamefunga , moja wa nguzo za uislamu. kila dini Huwa na Sheria na kanuni zake katika nchi. kuna baadhi ya dini kama vile wakristo, wahindi , waislamu na wakatholiki wote ni jamii moja. Sherehe za waislamu huongozwa na kadhi mkuu.

Bali na kuwa mwezi wa ibada matukio mengi ya kihistoria yalitikea wakati wa ramadhani, ambao ni mwezi wa Tisa katika kalenda ya kiislamu ya hijira ambapo ndani yake waislamu wamefaradhishiwa kufunga swaumukatika Hadithi zimeelezwa fadhila mbalimabali za mwezi mtukufu wa ramadhani.

Kufunga ni moja ya nguzo Tano za uislamu.mwislamu mzima , mwenye afya nzuri , anatakiwa kushiriki katika saumu ambayo ni ibada ya kufunga chakula au kinywaji mchana kutwa pamoja na kujizuia kufanya mapenzi toka alfajiri hadi magharibi na mke wako.isitoshe matendo haya ya Toba yanaendana na kuswali sana na kusoma Quran kwa wingi.

Neno Ramadhani inatokana na mzizi ya kiarabu ramid au ar_ ramad ambayo inamaanisha joto Kali au ukavu . mwisho wa ramadhani ni sikukuu ya idul fitri ambayo ni Sherehe ya furaha na kupongezana .waislamu wakati huu hutoa zahat na kuswali, baadaye hukutana kwenye karamu .katika ramadhani kwa wagonjwa, wanaosafiri, wazee , wajawazito, Wanaonyonyesha na wanawake wenye hadhi sio lazima kufunga siku ya ramadhani.

Mwezi mkuu wa ramadhani umetajwa kuwa mwezi wa kulikuwa yaani kuwa Katika ugeni.na mwenyezi Mungu, mwezi wa rehema maghufira ,baraka na machipuo ya Quran.kwa mujibu wa Hadithi .katika mwezi huu milango ya mbinguni na ya peponi hufunguliwa huku milango ya moyoni ikifungwa.
Kufanya ibada na kufunga saumu katika mwezi mtukufu wa ramadhani ni sehemu ya utambulisho wa waislamu.katika jamii za kiislamu Kuna ada, tamaduni na desturi mbalimbali kama vile kufanya marasimu na maneno ya kidini hafla za upatanishi hii hutokea wakati Kuna wale ambao wamekosana katika jamii au familia.wao hupika vyakula mbalimbali vya futari katika mwezi wa ramadhani na kadhalika.

Kuamsha watu kula daku.tangazo la kawaida wa swala na kuwaamsha watu kula kwa ajili ya kula daku ni mambo ambayo yamekuwayakifanyika tangu kale kwa mbinu mbalimbali .kama vile waadhini kuzunguka katika mitaa, kuwasha taa za chemil na kuzitumdika sehemu, kugonga milango kadha.


Katika jamii mbalimbali Kuna ada tofauti za kuwaamsha watu kwa ajili ya kula daku hasa maeneo ya vijijini . ramadhani ni mwezi ambao ndani yake, inasadikiwa kuwa wakati ambapo Qurani takatifu iliteremshshwa kutoka mbinguni kama mwongozo kwa wanawake na wanaume. Tangazo la uelekeo na pia njia mojawapo ya uovu kwa waislamu.katika mwezi huu waislamu hufunga mfungo mkali kuanzia alfajiri hadi machweo . ramadhani ni mwongozo wa maadhimisho ya dini au kituo Cha maisha ya kiroho.

Makosa wakati wa ramadhani. Akina mama wamekuwa wakishughulika majumbani kupika sana kiasi hata wanakosa muda wa kusoma Quran na kusikiliza darasa iwe masikitini au kwenye video.wakati wa mwezi mtukufu wa ramadhani waislamu hurundika vyakula majumbani na wakati huu wao hukaa na familia zao na kuongea na wanakula , hakuna aliyethubutu kuitisha kikao na familia na kuongea kuhusu ibada takatifu hii ni makosa zaidi.

waislamu wengi hufunga lakini nafasi zao hazibadiliki na kuwa ni wenye huruma na Imani kwa waislamu wenzao, umefunga lakini hujali kama Kuna waislamu wenzako ambao huhitaji futar .hata wakristo pia hufunga lakini baadhi Yao hawabadili tabia zao maishani mwao.

Wakati wa ramadhani ni Bora kufunga bila ya kujali kuwa ibada hii waislamu wengi hufunga kwa mazoea na hawana wasiwasi ya ibada zetu za kufunga zimebadilika, lakini ili kujiwekea mazingira ya kukubaliwa ni lazima kuwa na ghofu tunafanya na ukiwa na wasiwasi ni Bora kuamua kuacha.kila mwislamu anafaa kuswali vipindi vyote Tano.

Waislamu wengi hufunga kwa kuacha kula na kunywa lakini Bado huendelea na matendo yao kama kawaida. Mfano kusema uongo , kumengenya , kuiba , kudhulumu, kuzini baada ya na kadhalika.matendo haya hayafai siku zote lakini hafai zaidi ikiwa imefunga hapo ni sawa na kunywa maji kwenye kinu. Kufunga mwezi wa ramadhani Kuna faida nyingi kwa mwili.
Ni Bora kujitolea ili kuheshimu dini mbalimbali humu nchini, kwasababu bila dini jamii itakosa maadili.utengamano katika jamii husaidia jamii kuwa na amani kila wakati . waislamu hupika chakula kama vile buriani, wali na hata kula tende.

About The Author

Subscribe

- Never miss a story with notifications

- Gain full access to our premium content

- Browse free from up to 5 devices at once

Latest stories

spot_imgspot_img