9.6 C
London
Monday, May 20, 2024
HomeTravelUMUHIMU WA MATATU

UMUHIMU WA MATATU

Date:

Related stories

Why women struggle to take climate cases to court and how to correct it

By Pedi Obani A study in Nigeria and South Africa...

Calling off UN regional climate weeks exposes rich nations’ lack of goodwill

Funding these essential meetings would cost little to rich...

Kenya: Adding up the costs of the floods amid an economic crisis

The devastation from the floods in Kenya have been...

Can We Use ChatGPT for Global Goods Software Development?

At IntraHealth, where our mission is to support health workers...
spot_imgspot_img
Reading Time: 4 minutes

Matatu ni basi dogo linalobeba abiria mjini, hasa kwa safari fupifupi. Jina lingine la matutu huitwa daladala. Bali na kubeba , abiria, matutu pia hubeba mizigo kutoka sehemu moja hadi nyingine. Yafuatayo ni umuhimu wa matutu.
Matatu zimerahisisha usafiri . Raha ya kila mkenya ni kufika mahali anapenda . Ikiwa mtu Hana pesa za kulipia ndege Wala traini, basi , matatu itakuwa njia rahisi ya usafiri. Wanafunzi wanapoenda shuleni, baadhi Yao hutumia matatu kwasababu zimerahisisha usafiri wao. Matatu nyingi zimesaidia kukuza uchumwa nchini.Nchini kenya matatu huletea serikali pesa nyingi. Hi ni kupitia Kodi ambayo wamiliki wa matatu hulipa. Wakati mwingine matatu hutumika kusafirisha watalii kwenye mbuga za wanyama. Zile pesa ambazo watalii hulipa bila shaka husaidia kukuza uchumi wa nchi.

Matatu Hutoa ajira kwa watu wengi nchini kenya. Ni Bora vijana kutochagua kazi. Baada ya kukamilisha masomo, vijana wengi hutarajia kupata kazi ya ofisi. Hata hivyo ndoto Yao Huwa inakosa kutumia . Wakati wanazidi kusubiri kupata kazi waliyosomeaa, wao hubahatika kupata ajira kwenye sekta ya matatu. Sekta ya matatu huajiri wazee kwa vijana. Heko kwa sekta ya matatu kusaidia vijana kupata kazi.
Zimesaidia jamii kulisha familia. Kila familia unahitaji kukuzwa kwa njia ya ustarabu . Ni vyema kufahamu bila kufanya kazi, familia zetu zikakosa mahitaji maalum. Kwa hivyo matatu zimesaidia vijana kulisha familia zao. Kupitia hizo pesa ambazo wao hupata. Sekta ya matatu imeajiri madereva , utingo na hata kandawala . Bila matatu tungechelewa kufiika kazini, hata ratiba za shule zingechelewa.

Ni Bora kufahamu kuwa jambo nzuri lazima pia liwe na kasoro. Si kila jambo huwa la manufaa hadi mwisho. Matatu Huwa na changamoto zifuatazo
Matatu zimesababisha ajali nyingi nchini pamoja na vifo vya watu.utapata kuwa baadhi ya watu huzaliwa wakiwa buheri wa afya . Lakini wanapotumia matatu kama chombo Cha usafiri, kwa bahati mbaya ajali hutokea . Jambo hili husababisha ulemavu baada ya kupatwa na ajali. Wengine hata huenda wanapoteza maisha Yao kighafla. Mfano wa kupigiwa upato ni ajali ambayo ilitokea huko Londiani ambapo watu wengi walipoteza maisha Yao.
Ajali barabarani husababishwa na mwendo wa Kasi. Barabara mbovu, elimu duni kwa madereva wengine huendesha gari wakiwa walevi. IIi kuepuka ajali hizi, ni Bora kuzingatia Sheria za barabarani.

Matatu hizi husababisha Hali ya msongamano wa magari mjini. Mtu akitoka nyumbani, ana matumani kufika kazini au shuleni mapema. Katika mji mkuu kama, Nairobi, msongamano wa magari ni kero kuu. Magari yanapoenda kwa mwendo wa kinyonga. , Hali hii kwa mara nyingi huchelewesha wale ambao wanaenda kazini. Watu hupeleka bidhaa zao sokoni, kwasababu muda wao wote hupotelea wakati Kuna msongamano almaarufu ” jam ” barabarani.
Si ajabu kusikia kuwa matatu zimetumika katika usafirishaji wa bidhaa za magendo. Katika nchini jirani ya Uganda, watu wengine nchini kenya hutumia matatu kupelekea bidhaa za magendo, wao hawaogopi huenda watakabiliwa na mkono wa Sheria. Bidhaa za magendo ni kama Bangi , katika maeneo ya Teso kusini bidhaa gushi kama pombe husafirishwa. Kule maeneo ya koteko kulikuwa na kisa Cha ajabu sana, Kuna afisa wa polisi alifariki baaada ya kugongwa na gari. Gari hili lilikuwa limebeba bidhaa za magendo. Dereva wa gari hili alitaka kuhepa kutiwa mbaroni.kwa hivyo aliamua kutolipia ushuru na kutumia njia ya mkato, susababisha kifo. Pole kwa afisa huyu wa polisi kwa kuiaga Dunia akiwa kazini.


Matatu zimechochea ufisadi chungu nzima kwa askari wa trafiki huchukua hongo, matatu Huwa na shida nyingi mno, Kama vile ukosefu wa breki. Labda dereva amepatikana akiendesha gari kwa mwendo wa Kasi. Yule afisa wa polisi , badala ya kushika Hilo gari yeye huchukua hongo. Ufisadi bila shaka , imechangia ajali barabarani. Ni Bora askari kuepuka kuchukua hongo wakifanya hivyo matatu zotapunguza ajali barabarani.
Madereva pamoja na baadhi ya kondakta , utingo hutumia lugha chafu, au matusi kwa abiria. Hali hii hutokea wakati wa kurudisha Salio au change akiulizwa huanza matusi kwa abiria. Wakati mwingine hata husababisha vita vya wenyewe kwa wenyewe. Si vyema wao kutumia matusi kwa abiria kila siku . Wakati pia dereva anaambiwa kupunguza sauti ya muziki, anaanza kutoa cheche za maneno.
Kutokana na vifo vya watu wengi , jamii huachiwa jukumu la kuwatunza wajane, walemavu na mayatima . Gharama yote huachiwa majeruhi.ikiwa hawajipanga na bima ya afya huenda utawapoteza wapendwa wako. Hali hii hurudisha nyuma maendeleo katika jamii na kuzima ndoto ya wengi. Madereva wanafaa kuwa makini sana barabarani.
Baadhi ya matatu hubeba watu kupita kiasi. Hali hii huathiri usalama barabarani. Si ajabu kusikia utingo wa gari la “super metro” ilipoteza utingo wake kupitia ajali ya barabarani. Pia katika gatuzi la Nairobi kuliripotiwa kuwa na shida ya kunguni. Wadudu Hawa walipatikana kwa magari ya matatu. Sababu kuu ni kuwa baadhi ya matatu Huwa chafu na hatimaye huhifadhi kunguni wengi.

About The Author

Subscribe

- Never miss a story with notifications

- Gain full access to our premium content

- Browse free from up to 5 devices at once

Latest stories

spot_img

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here