6.2 C
London
Saturday, April 27, 2024

Faida za Mnazi

Date:

Related stories

Tamasha Ya Muziki.

Wakuza mitaala wa humu nchini wamejadili vilivyo jinsi ya...

Kenyan Doctors Reject Government Offer, Strike Continues Over Internship Issue

In a recent development, the doctors' union in Kenya...

Delegates Convene for Talks on Plastic Pollution

Delegates during the official opening of the Third Session...

Government and Doctors Nearing Deal as Talks Extend to Tuesday

In an encouraging update, Head of Public Service Felix...
spot_imgspot_img
Reading Time: 4 minutes

Ilikuwa ni jambo la kuvunja moyo kule katika kaunti ya kirinyaga. Hii ni baada ya pombe ya haramu kuua watu watu wengi sana. Gavana wa kirinyaga Bi Ann Waiguru aliamurisha baaadhi ya baa au danguro mia tatu zifungwe. Ilibidi waziri wa usalama bwana kithuri kindiki kupiga marufuku pombe haramu kote nchini. Leseni zote za baa nchini zilifutiliwa mbali, halafu ukitaka kufungua biashara yako ni lazima utume maombi ya leseni mapya tena. Mfanyikazi wa umma aliyemiliki baa lazima afunge baa hiyo au awache kazi serikalini.

Pombe haramu iliharibiwa na kumwagua katika kaunti mbalimbali.Naibu wa rais bwana Rigathi Gashagua alisisitiza kuwa hatalegeza azimio lake ya kupiga pombe haramu humu nchini kenya .kule mombasa wakaji wanadai kuwa mnazi si pombe haramu na wanashangazwa ni kwa Nini serikali inataja mnazi kama pombe haramu.Huku muratini ikishabikiwa kuwa pombe si pombe haramu baada ya mahakama kutoa kauli ya mwisho kutetea pombe hii. Hata hivyo pombe ya mnazi Ina faida chungu nzima , kama ifuatavyo.

Mnazi ni mojawapo ya miti inayostawi katika eneo ya pwani na huwafaa na kuwakidhi wakazi wa kaunti ya Mombasa katika shughuli za kuinua uchumi wao. Wanapouza pombe hii wao hupata kitega uchumi kama riziki ya kuwasomesha watoto wao katika shule mbalimbali.mnazi hutengenezwa kutoka na maji ya Nazi na kinywaji hiki hupendwa zaidi na wakaji wa pwani.mara nyingi wakati wa sherehe watu hunywa mnazi kama kufurahisha nafasi zao.mti wa mnazi inaweza kutumiwa kujenga nyumba na mzizi wa Nazi hutumiwa na wakaji wa Mombasa kama dawa ili kutibu maradhi kadha wa kadha.Ni vyema kufahamu kuwa mti wa mnazi hutumiwa kutengeneza mafuta ambayo hutumika katika shughuli za mapishi kula jikoni, huku nyumbani mafuta ya urembo , mafuta ya nywele, nishati inaweza kutengenzwa kutumia Nazi .mnazi unajulikana kwa jina jingine “kalpa” kumaanisha mti ambao hutupatia mahitaji maalumu ya kuwaezesha kuishi maisha Bora.

Pombe ya mnazi unajulikana kwa majina kadha ya kienyeji, ni kinywaji chenye kileo kilichoundwa kutokana na mnazi .pombe ya mnazi Ina lishebora kama proteini , wanga , amini acidi na vitamini kama vile B 3 na c za madini kama vile zinki na magnesium.pombe ya mnazi pia hupatikana katika masimulizi ya kale kale .mnazi husaidia mwili kuzuia viini kutoka na kuharibu seli mwilini ambayo hupambana na maradhi ya saratani.

Pombe ya mnazi husaidia Neva na misuli kufanya kazi kikamilifu.kama tujuavyo mshipa hii Ina joto na huhakikisha kuwa mipigo ya moyo imetiliwa mkazo .pombe hii ni Bora kwa wale ambao wanaugua kisukari.nywele zenye afya hutengenezwa kutumia pombe ya mnazi .mnazi hutokana na mimea ya ” palmae” chimbuko lake ni kutoka Asia ya kisini lakini imesamba katika Karne mbalimbali, mbegu ya mnazi huzaa baada ya kukaa kwenye maji ya bahati kwa muda Fulani. Hivyo basi mnazi inapatikana pwani katika sehemu baridi baridi. Watu walipenda kubeba mnazi safarini kwasababu ni chakula.pombe ya mnazi inasaidia kuzuia kuzota kwa misuli.huweka macho kuwa na unyevu kupunguza mkazo wa macho kwa muda.

Mkwenzi ni mtu anayefanya kazi kupanda miti aghalabu mnazi na kuagua Nazi . Mtu mrefu unaotoa matawi yenye majani marefu yanayotumika kujengea .watu hupata matunda yanayoitwa Nazi.
Kwa mara nyingi hutumiwa kupikia vyakula au kutengeneza mafuta.pombe ya mnazi huuzwa Afrika mashariki ikiwemo Tanzania na kenya ,magharibi mwa Afrika kwa mfano huko Nigeria, Ghana, china na Cameroon. Mnazi huzaa Nazi kila mwezi .kilimo Cha mseto wa minazi na mazao mengine humwongezea mkulima chakula kingi shambani. Watu hutumia makuti katika ujenzi wa nyumba na mapishi ya Nazi kama vile maharagwe ya Nazi Huwa tamu kama asali .mti wa Nazi kuishi umri wa wastani .makuti pia hutumika kama kivuli wakati Kuna jua kali mno .kifuu Cha Nazi kinaweza kutumika kama mapambo kama vile herini,bangili na vidani na mapambo mengineyo majumbani na kuwa kivutio kikubwa. .kifuu pia hutumika kama dawa ya kutoa sumu mwilini mwa binadamu kila wakati.

Machicha za Nazi hukaushwa na kutumika katika kutengeneza sabuni sabuni za aina mbalimbali za kufulia au kuogea .kuku hupenda kula machicha ya Nazi .mnazi hufanya mazingira kuwa na madhari ya kuvutia.mnazi ni mti ambao unastawi zaidi katika maeneo ya Tanzania kule visiwani kama vile mafia na unguja maeneo mengine mengi zaidi.nazi hupatia mafuta mazuri ya kupaka mwili zetu kila mara .mafuta hii ya Nazi huuzwa katika maduka ya jumla mjini kenya.pombe ya mnazi pia Huwa na changamoto pia Bali na uzuri wake ikiwa wewe ni mjamzito si Bora kunywa pombe . wanawake katika umri miaka Yao ya uzazi ambao wako katika mzunguko au kabla ya hedhi wanapaswa kufahamu kuwa pombe hulewesha haraka zaidi nyakati hizi.
Baadhi ya vinywaji vya pombe vinaweza kuwa Bora zaidi kuliko vingine.Hii ni kwasababu huathiri sukari ya damu na Kuna uwezekano mdogo wa kuzudisha uchovu .kwa kweli baadhi ya vinywaji vya pombe vinapotumiwa kwa kiasi kikubwa Huwa na madhara mwilini.mwacha Mila ni mtumwa, tukiacha pombe ya mnazi tutakuwa watumwa .

About The Author

Subscribe

- Never miss a story with notifications

- Gain full access to our premium content

- Browse free from up to 5 devices at once

Latest stories

spot_img

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here