10.6 C
London
Friday, October 18, 2024
HomeEducationFAIDA ZA KUVALIA SARE ZA SHULE

FAIDA ZA KUVALIA SARE ZA SHULE

Date:

Related stories

African Peacebuilding Network: Individual Research Fellowships

The APN and Next Gen program of the Social...

Applications for IOC Young Leaders Programme 2025-2028 now open

Applications for IOC Young Leaders Programme 2025-2028 now open Young...

Turmoil in Kenyan Politics; National Assembly Votes to Impeach Deputy President.

In a stunning development that has sent shockwaves through...

How Can African Women Bridge the Digital Gender Gap?

By Guest Writer There is a harsh reality in digital development:...

Man, 47, jailed for FGM in Nottingham

The UK is making strides in sending perpetrators of...
spot_imgspot_img
Reading Time: 3 minutes


Sare ni nguo zinazofafana zinazovaliwa na kikundi Cha watu . Kwa mfano wanafunzi , wafanyikazi au askari . Timu za mipira pia huvalia gezi maalum . Kuna aina mbalimbali za sare za shule nchini kenya . Kila shule imechagua sare ambayo ni ya kipekee kutokana na sare za shule nyingine . Sare za kipekee zinasaidia kujenga umoja wa wanafunzi . Mara nyingi sare za shule hushonwa kutumia rangi za shule. Pia shule ya shule inaweza kushonwa juu ya sare hiyo, kama vile baji.

Ingawa serikali ya kenya Inatoa elimu bila malipo . Kuna Karo nyingi kama vile sare . Kila mwanafunzi lazima awe na sare moja kuvaa wakati wa hedhi au wakati wa siku mbalimabali. Kama mwanafunzi anakuwa mkubwa , atahitaji kununua sare nyingine.
Kwa wasichana, sare za shule hujumuisha shati au blausi , sweta au kibao , sketi au kaptura , tai na nguo , vitabu na soksi . Sare ya shule inaweza bado kuonekana tofauti wa mwanafunzi mmoja hadi mwingine . Zaidi ya miaka ishirini iliyopita sare za shule zimekuwa biashara kubwa. Shule zingine ambazo zimetekeleza wajibu wa kuvalia sare zimechangia kile ambacho kawaida hufukiria kuhusiana na shule za kibinafsi . Baada ya kujadiliana na wazazi ni Bora kuteua sare rasmi ili kuleta utangamano katika jamii .

Sababu za sare za shule zinazingatia ufanisi wao katika mazoezi . Maelezo ya awali kutoka kwa watendaji katika shule ambazo zimetekelezwa zinaonyesha ukweli kwamba Wana athari nzuri ya nidhamu na shule.
Zinatoa mazingira salama ya shule. Kwa kuwa wanafunzi wote wamevalia sare , inaweza kuwa rahisi kubainisha ni nani hatakiwi kuwa humo. Hili pia huzuia wanafunzi kuonyesha mfungamano wao na magenge kwa kuvaa rangi Fulani au nguo Fulani.


Sare huruhusu wazazi kuweka akiba kwa wakati na pesa zinazotumika kununua nguo za shule , kwa kawaida sare za shule inaweza kuvaliwa kwa mwaka mzima au miwili .mzazi hatakuwa na mzigo wa kununua sare kila siku.
Wanakuza roho ya shule . Sare hukuza fahari . Wakati kila mtu amevaa sawa anajihisi kuwa na fahari . Jambo hili huongeza ari mwilini wa mwanafunzi , anahisia kubwa zaidi ya umoja za kiburi. Sare huondoa utengano wa kijamii . Jinsi unavyovaa kwa kawaida huamua ni aina gani ya mtu, ikiwa kila mtu amevalia sawa, inaweza kuondoa hitaji la kuweka ” lebo” kwa kila mtu na mwekekeo wa kushikamana na umati wako.

Sare za shule hutengeneza usawa. Wanafunzi wanapovalia sare kinaweza kuwa na Hali ya umoja kwasababu kila mtu atavaa nguo sawa na Wana utambulisho mmoja . Sare itaondoa ushindani mdogo kati ya watoto kuhusu nani ana mavazi ya Bei ghali zaidi au nani anaonekana Bora zaidi kuliko mwingine shuleni.
Sare ni njia moja ya kuwahiza wanafunzi kujieleza kwa njia nyingine . Kwasababu watoto hawataweza kuonyesha ubinafsi wao kupitia nguo, watajaribu kujieleza kupitia njia zingine kama Sanaa , wasomi, michezo au shughuli za Ubinafsi zaidi . Shuleni watazungumza lugha moja na bila shaka huleta utangamano. Wanazuia uonevu , sare za shule inaweza kusaidia kukomesha suala la uonevu . Jinsi watoto wanaovaa tofauti au wasioweza kununua nguo zenye chapa wanafanyiwa, mzaha na kubaguliwa.

Hata hivyo sare za shule Huwa hasara zifuatazo, baadhi ya sare hufanya wanafunzi kutovumilia tamaduni. Sare nyingi hazijaundwa kulingana na mavazi ya kutamaduni ya idadi ya watu au zitawakilisha utamaduni mmoja tu.ikiwa watoto huenda shuleni siku tano au sita. Kwa wiki . Wazazi wanahitaji sare angalau tatu. Jambo hili linaweza kuwa ya gharama tatu. Jambo hili linaweza kuwa ya gharama zaidi kwa mzazi.
Sare husababisha kinyongo mioyoni mwa wanafunzi . Kwa hivyo kuwahitaji wanafunzi kuvaa sare ni kinyume na matakwa Yao kunaweza kusababisha chuki, dhidi ya shule na hata wazazi . Watoto wanapokuza maoni Yao wenyewe , hawatafurahia , kulazimishwa kufanya jambo ambalo hawataki.
Wasichana wanauzoefu wa kunyanyaswa kwasababu ya urefu wa sketi zao. Kwa hivyo wao wana hofu , kuhusu ubakaji wanapotembea . Shuleni Kuna wale wanaotaka wasichana wavae sketi ndefu na wale ambao wanaofikiria urefu wa sketi za wasichana si jambo la kutilia mkazo . Jambo la kusikitisha ni wasichana wakibakwa ama kuchokozwa kwasababu ya sketi fupi lawama Huwa kwao.

Kwa kuwataka wanafunzi wavae sare zinazofafana, shule huondoa mvutano unaotakana na mitindo na majina ya bidhaa. Sare pia hukosea wanafunzi wa kike heshima. , kwasababu hata wakiwa wajawazito ni lazima wavalie sare rasmi ya shule. Kwa jumla sare hupunguza matukio ya uonevu , vurugu za chuo kikuu na hutoa mazingira ya kusomea katika makazi .

About The Author

Subscribe

- Never miss a story with notifications

- Gain full access to our premium content

- Browse free from up to 5 devices at once

Latest stories

spot_imgspot_img