11.8 C
London
Saturday, October 5, 2024
HomeCommunitySiku Ya Wakimbizi Turkana

Siku Ya Wakimbizi Turkana

Date:

Related stories

Man, 47, jailed for FGM in Nottingham

The UK is making strides in sending perpetrators of...

Vumbi Ni Hatari Katika Afya yetu?

Vumbi ni hali ya chembe zinazopeperuka hewani za asili...

Fahamu Zaidi Alama Za Barabarani

Alamu za barabarani huweza kuwa nguzo muhumu kwenye kando...

Hofu Yatanda Kufuatia Mlipuko Wa Mpox

Ugonjwa wa Mpox husababishwa na virusi vya "Monkey Pox"...

Je, Kamusi Inatofautiana Vipi Na Vitabu Vingine?

Shuleni ni mahali ambapo wanafunzi huenda ili kupata elimu....
spot_imgspot_img
Reading Time: 4 minutes

Je, mkimbizi ni nani? Mbona nchi hushuhudia idadi kubwa ya wakimbizi.Si rahisi watu wengi kutoroka kutoka katika makazi yao, labda k sababu mbalimabali ambayo huchangia kuibuka kwa wakimbizi hawa, hata hivyo watu ambao wanalazimika kukimbia nchi yao na kutafuta usalama katika nchi nyingine ni wakimbizi . Hawawezi kurudi katika nchi yao kwasababu ya kuteswa kwa hofu kutokana na nini wanachoamini au kusema, au kwa sababu ya migogoro ya silaha , vurugu au machafuko makubwa ya umma.

Mtu anayetambulika kama mkimbizi atakuwa na haki ya kuajiriwa, kuanzisha biashara au kufanya taaluma au biashara fulani.Mkimbizi ana hofu iliyojengwa ya kuteswa kwasababu ya rangi , dini , utaifa maoni ya kisiasa au uanachama katika kundi fulani la jamii .
Shirika la umoja wa mataifa la kuhudumia wakimbizi (U.N.H.R.) lilipongeza Kenya kwa uungaji mkono wa mshikamano wake unaoendelea ambao umekuwa muhimu katika kutoa hifadhi kwa wakimbizi. Aidha wakimbizi walio katika kambi hupatiwa msaada wa fedha , chakula na nguo kutoka kwa wahisani tofauti nchini.

Ni vyema kuwapongeza mashirika mbalimbali ya kijamii ambayo yamekuwa mstari wa mbele kutoa msaada tofauti kwa wakimbizi hao na kuwataka kuendelea na moyo huo huo wa kutoa usaidizi katika kaunti ya Turkana .Pia wakimbizi hupitia shida nyingi kama vile msukosuko wa kisiasa ambayo hupelekea wao kupoteza maisha yao kighafla.Tukumbuke kuwa usaidizi unaotolewa kwa hiari kwa wakimbizi ni ishara ya utangamano na umoja katika jamii nzima .

Wenyeji wa Kakuma , Sessi, Mayie , hujitolea kwa hali na mali kuhakikisha kuwa wakimbizi wamepata usaidizi wa kutosha tangu kuwasili kwao.Marekani ilitoa msaada kwa wakimbizi wa Moyale.Abdi Gonjbe alidokeza kuwa msaada huo ulitokana na taarifa zilizopeperushwa kote duniani kuhusiana na hali ya wakimbizi Moyale.

Wakimbizi kama ilivyofafanuliwa na U.N.H.R. na serikali ni kuwarejesha wakimbizi kwa hiari yao kwenye nchi zao za asili .Kuwajumuisha ndani ya ukimbizi na kuwapa makazi katika nchi ya tatu . Wakimbizi huweza kupatikana Sudan, Iraq na mamlaka ya kitaifa ya Palestine.Nchi yenye idadi kubwa ya waliohamishwa makwao nchini mwao ni Sudan ambapo idadi hiyo ni watu milioni Tano. Wakazi wote walipohesabika .

Azerbaijan ilikuwa na idadi kuu ya watu waliofukuzwa kutoka makwao ulimwenguni kote. Wakimbizi ambao huhama nchi zao hutafuta Ukimbizi katika nchi jirani na kwao.Suluhisho la kudumu kwa idadi kubwa ya wakimbizi kama ilivyofafanuliwa na U.N.H.C.R. na serikali ni kuwarejesha wakimbizi kwa hiari yao kwenye nchi zao za asili. Kuwajumuisha ndani Kuna mapatano ya kimataifa yanayoratibu hali hiyo.Chini ya mkataba ya umoja wa mataifa kuhusu hadhi ya wakimbizi.

Mkimbizi ni mtu ambaye hutoroka nchi yake kwasababu ya rangi, dini, utaifa , uanachama wa kikundi fulani cha jamii au maoni ya kisiasa , yumo nje yake na ameshindwa au kutokana na hofu hiyo, Hana nia kutegemea ulinzi wa nchi hiyo .Katika Afrika na Amerika ya kilatini. Kuwajumuisha watu waliokimbia vita au vurugu vingine katika nchi zao za asili . Mkimbizi ni mtu aliyeondoka kwao kwasababu ya kulazimishwa.

Baadhi ya wakimbizi wanaoishi katika kambi ya wakimbizi ya Kakuma kwenye kaunti ya Turkana wamekerwa na mpango ya serikali kusema kwamba kambi hiyo itafungwa ifikapo mnamo mwezi Juni .Kenya ina zaidi ya wakimbizi elfu mia saba kwenye Sehemu ya kaskazini kwa nchi, baada ya wadau wakuu kupitisha rasmi mpango wa kuwaingiza kwenye jumuiya za wenyeji.Wakimbizi hao aidha wanadai kwamba migogoro katika mataifa yao iliyowasababisha watoroke bado wanaendelea hivyo hatua ya kuwataka kurejea inahatarisha maisha yao.

Bwana Bitok amesema katika taarifa iliyotolewa mjini Nairobi.Wakati wa Kuadhimisha siku ya wakimbizi duniani.Kwamba lengo la sasa ni kuhakikisha rasilimali inafikia wanachi ili kutekeleza mpango wa shirika , huku awamu ya kwanza ya mradi wa miaka minne ikikadiriwa kugharamia dola milioni.

Wakimbizi hao wamependekeza kupelekwa katika mataifa mengine yenye usalama badala ya kurejeshwa nchini mwao .Hizi hapa hisia za baadhi ya wakimbizi wao.U.N.H.C.R. aidha inataka Kenya kuwapatia vitambulisho vya kitaifa wakenya elfu kumi na moja , waliojisajili kuwa wakimbizi kwa lengo la kupata msaada. Kenya imeweka mpangilio ya kuwawezesha wakimbizi kuishi katika mataifa mengine ya Afrika sehemu nyingi Nchini.

Ni jambo la kutia moyo sana humu nchini.Itakumbukwa kwamba Kenya na U.N.H.C.R. zilifikiana kuhusu masuala muhimu yanayostahili kutekelezwa kabla kambi hizo kufungwa katika mafanikio haya ni kwamba Kenya ifanikishwa kuwarejesha katika nchi zao , wakimbizi hao kuwa Wana usalama.

Makazi ya wakimbizi ya Kalobeyei, mradi uliozinduliwa mwaka wa elfu mbili na nne, ili kutekeleza azma ya kuwawezesha wakimbizi kujitegemea, kujumuisha katika huduma za kitaifa na kutumia pamoja na wenyeji ili waweze kuhudumia jamii nzima .

Joel Mkimbizi kutoka Burundi ana duka la kunyoa nywele na pia vipodozi.Mpango wake Mwakanini kununua vifaa vingine vikubwa vya kunyolea ili ifikie kiwango anachotaka.Irene Kai mwenyeji mjasiriamali anaonekana akiwasha taa iliyounganishwa kwenye mradi wa nishati ya sola huku akiweke vinywaji kwenye jokofu.

Wafanyabiashara na wakimbizi na Wana Imani Nai.Sasa tufanye biashara na wakimbizi. Na tangu sasa umeme umefanya kazi yetu imekuwa rahisi.Bwana Grandi alipatiwa maelezo kuwa mradi huo wa sola unaofanikishwa na benki ya Dunia imewezasha wakimbizi hao kujikimu kiuchumi.

About The Author

Subscribe

- Never miss a story with notifications

- Gain full access to our premium content

- Browse free from up to 5 devices at once

Latest stories

spot_imgspot_img